CALVIN AND ALVIN… Mtunzi:Steven George SEHEMU YA MWISHO - TopicsExpress



          

CALVIN AND ALVIN… Mtunzi:Steven George SEHEMU YA MWISHO Ilipoishia Nilisita kidogo kujitokeza jikoni,nikajibana kwa pembeni nikiwasikiliza “aaaahh wapi mama wewe najua kwa kumsifia tu kaka hujambo, ukute huyo mwanamke Asha boko tu mzuri” “hahaha usimchezee kaka yako wewe, wale ndo wakwe ninao wataka mimi sio wewe unaokota mahousegal huko wanakuja kunichafuria sofa zangu humu ndani” “kwani huyo mwanamke yupoje mama….” “eehh mzuri huyo zaidi hata ya yule Diana mtangazaji” “kwani anamzidi yule wangu ambaye baba alimfukuza siku ile?” “ule mbona uchafu tu, huyo mwanamke kumuelezea mie siwezi ila anaitwa nani vileeee…Prisca sijui Krista…..” mama alisema jina huku akijifanya kama hana uhakika nalo “Prisca? Prisca yupi huyo?”Alvin alimuuliza mama huku akishangaa na kumsogelea karibu “mie sijui ila kama unamfahamu ndo huyo huyo mtoto mweupeeeeee kama mama yenu” “we mama acha masihara huyo Prisca anamwanya?” “mhh sikumuangalia vizuri..ila anashepu shepu hivi halafu mtoto wa watu kajaaliwa dimpozi juu” “aaaahh mama ngoja…..?????” “Ningoje nini?” Alvin hakuendelea kusema chochote zaidi ya kutoka pale akitaka kunifuata chumbani ili aje kuniuliza lakini Face to face alikutana na mimi nikiwa nimesimama pembeni nikiwasikiliza… SASA ENDELEA Baada ya Alvin kuniona nimesimama pale mlangoni nikimuangalia huku nikiwa nimetulia tu nimejishika kidevu alikuja karibu yangu na kuniuliza haraka haraka “Bro demu gani eti alikuja?” “mke wangu alikuja” nilimjibu kwa kujiamini na kwa pozi flan “huyo emu demu yupi?” “kwani jana uliongea na demu gani kwenye simu yangu?” “ndo huyo? Sasa mbona mama anasema eti amekuja Prisca” “Ndio kaja Prisca, ila sio Prisca wako ni Prisca wangu mimi” “Bro acha kunivuruga bhana hebu njoo chumbani huku tuongee vizuri” Alvin alinivuta mkono na kunipereka hadi chumbani na kuniomba nizungumze naye kumpa habari kamili ya huyo manzi… “Bro ujue unanichanganya kabisa, yaani sikuelewi elewi..hebu niambie tena vizuri, Prisca huyo yupoje?” “usitake kujua Prisca huyo yukoje, nimekuambia ni prisca wangu ambaye nilimpata hapo nje alikua anakatiza mitaa mie nikamuungia …” “ujue mama alivyonielekeza naona kama ni yule Prisca wangu” alisema Alvin kwa upole kidogo Nilimuangalia alivyokua anapresha ya kutaa kujua ukweli lakini sikutaka kuwa na haraka ya kumwambia lolote juu ya hilo, “Kwani Prisca wako vipi mbona haunipi habari zake?” Nilimuuliza Alvin kuhusu yule demu ambaye alimtumia elfu hamsini na kunidanganya kwamba daily huwa anaonana naye.. “demu nipo naye kama kawaida bro na hivyo kesho kasema anakuja” Alvin aliendelea kunidanganya, hakutaka kuweka wazi kwamba yule mwanamke ambaye alimtumia hela hakuwa Prisca kweli hivyo katapeliwa, mie niliendelea kuongeanae kwa kujiamini huku nikiweka pozi kama kawa.. Kiukweli Prisca nilikua tayari nimeshampenda ila baada ya kuniambia yeye ni mwanafunzi basi nilichoka kabisa na ile hamu ya kumpenda tena haikuwepo, moyo ulikufa ganzi, nilifikiria nimuachie tu Alvin aendelee naye lakini kwakua Alvin alikua ni jeuri sana nikahisi atamvuruga tu mtoto wa watu na kumfanya asiendelee na masomo na kama ataendelea basi akili ya Prisca inaweza ikavurugika kwasababu hakuna mapenzi na shule,… “kwahiyo dogo huyo Prisca wako anakuja kesha sio?” “yap kesho anakuja….ila niambie Prisca wako anakaa wapi?” “Prisca wangu anakaa mbagala” nilimjibu Alvin huku nikimficha ukweli kwamba prisca anakaa usalama “aaahh kama wa mbagala basi sio wangu huyo, mie wangu anakaa usalama pale magomeni” alisema Alvin huku mie nikimcheka kimoyomoyo… Baada ya kumaliza kuongea hayo Alvin alienda zake kuoga na mie nikaenda zangu sitting Room kwaajili ya kuangalia Tv huku akili yangu ikiwaza jumatatu kwenda kuripot chuo, nikiwa nipo naangalia Tv yule mwanamke akatuma meseji kwenye kisimu changu cha Tochi “Calvie nikuambie kitu” “yap Prisca niambie” “hapa mwenzio nakuwaza kweli, nimekaa tu chumbani naiangalia hii Tshert uliyonipa” “acha utani bwana unaniwaza nini sasa?” nilimuuliza P “mie sijui nakuwaza nini ila elewa nakuwaza” “okey P thanx” “mmh haya, unafanya nini?” aliniuliza Prisca “naangalia Taarifa ya habari” “upo na mama nini?” “hapana nimekaa na Alvin tu” nilimjibu Prisca nimekaa na Alvin wakati nilikua nimekaa pekeyangu, nilimwambia vile ili nione atasema nini “mmmh Plz naomba ukisoma text yangu futa asije akakununia huyo” “usijali P nipo makini na simu yangu” Nilimjibu Prisca kisha simu nikaiweka pembeni nikakazia macho kwenye Tv baada ya kuona taarifa moja matata sana kwenye tv ambayo ilikua inasema watu watatu wamechomwa moto mkoani msoma wakidhaniwa ni wachawi, watu hao ni familia moja wakihusishwa kuwa ni dada, mjomba na mtoto mdogo mwenye umri wa miaka 16… Nikiwa nipo makini kusikiliza habari hizo kumbe Alvin alikua ametoka bafuni tayari akawa amekaaa pembeni yangu akiwa ameshika simu yangu ile ya tochi akiichezea chezea” duuuhh bro hiki kimeo bado unacho tu?” “tulia bwana nasikiliza habari muhimu” nilimwambia Alvin huku nikiendelea kutolea macho tv bila kujua Alvin kama kashika simu yangu na kaanza kuichokonoa chokonoa, Kumbe wakati ameishika ile simu kulikua na meseji kutoka kwa Prisca iliyosomeka “kama vipi tutafute sehemu tu nyingine tuwe tunaonana mie kuja tena hapo sitoweza, nitamuonea aibu Alvin ukichek simu zake sipokei nishaanza kumpotezea” Alvin alishtuka kidogo baada ya kuona ile meseji, akaunganisha na tukio lake la kupigwa elfu hamsini basi akajua ndo Prisca yule yule ambaye alimtapeli kumbe sio, matukio tu yalifanana kwasababu Alvin ambaye anawasiliana na Prisca ni alvin feki sio arijino na Demu ambaye anawasiliana naye Alvin sio Prisca orijino ni feki halafu ukichek Alvin kila akipiga simu anazinguliwa na yule demu aliyemlia hela kwa kutopokea simu yake… Alvin alipandwa na hasira alitaka aje juu palepale lakini akawa mpole, akachukua namba ya Prisca bila kuniambia, na alipoona ile namba imeishia 25 ndo akajua ile ndo namba orijino ya P, baada ya mimi kumaliza ile habari uchawi nikamgeukia Alvin na kumuuliza ulikua unasemaje? Alvin aliniangalia tu usoni huku akinipa simu yangu ya Tochi huku ile meseji aliyotuma Prisca akiwa ameifungua na kunionyesha, Nilikaa kimya bila kusema chochote zaidi ya kuipokea na kuiangalia tu,mbaya zaidi Prisca nilimsave kwa jina lake kamili tena nikiongezea na jina la maeneo anayokaa “Prisca magomeni” Nikiwa sijui niseme nini Alvin aliinuka pale kwenye sofa na kuelekea chumbani kwa kasi sana…. Aliniacha na mawazo pale kwenye kochi, nilijaribu kufikiria na kujiuliza au nimwambie Prisca? Nikaona ni upumbavu mtoto wa kike kutaka kutugombanisha mie na ndugu yangu hivyo nikainuka na kumfuata Alvin chumbani, nilipoingia chumbani nilimkuta Alvin analia, nilishindwa kumsemesha zaidi ya kukaa kimya na kumuangalia tu huku kichwani zikinirudia zile kumbukumbu za siku ambayo nilikua nalia mimi baada ya Diana kunitumia txt kalazwa, nilikosa cha kusema na ndipo Mungu baba akaichukua akili yangu na kuipeleka kwenye neno la mungu ambalo lina sema “ANAYECHEKA LEO, ATALIA KESHO” Neno la mungu linamaana kubwa sana kama utalisoma na kulielewa, nadhani unakumbuka vizuri sana siku ile ambayo mimi nilikua nalia Alvin alinicheka sana hadi akaenda kumwambia mama, na yeye leo analia je nikamwambie mama?? Ushauri wangu wa bure kwako ndugu msomaji “usimcheke yule ambaye anakuja kwako na kukuomba shilingi mia, kama unauwezo basi msaidie na kama hauna uwezo basi mpe moyo atapata na sio kumcheka” Alvin kwa mara ya kwanza nilimuona akidondosha chozi kwaajili ya mrembo Prisca ambaye bado ni mtoto mdogo sana lakini kaanza kuitikisa nchi juu ya uzuri wake, Ametufanya tumsahau Diana, alinifanya nivunje ukuta imara ambao nilikua nimeujenga ndani ya moyo wangu, nilikua sina budi kuufanya moyo wa alvin utulie hivyo nikamsogelea Alvin na kumshika bega “hebu niambie ukweli maana naona unanidanganyaga tu, hivi ushawahi kuonana na Prisca toka utume ela siku ile?” Nilimuuliza alvin lakin hakunijibu kitu zaidi ya kwikwi tu nyingi za vilio, niliendelea kuongea naye “mdogo wangu Prisca yule unayewasiliana naye na kumtumia pesa ni Prisca feki ila unajifanya mjanja na kunidanganya eti Prisca mambo yako poa soon tu mtoto anaibuka geto, mara oohh eti nilikuanae leo, acha zako dogo” “kaka ni kweli nilikua nakuambia nipo naye ila ule ni uongo tu ili nikutamanishe” “sasa huko kunitamanisha kwako kumefikia wapi? Si unaona umepigwa na hela juu” “bro namba si ulinipa ww” “nilikupa namba au simu uongee na yule mtu ambaye alikosea namba? Kwaujinga wako ukajikologa mwenyewe na kuanza kulopoka Prisca nambie, mimi ndo Alvin tuliyekuata pale sinza…sasa demu akakuona wewe limbukeni wa mapenzi na ndomaana akakuingiza mjini, eti wewe mwenyewe ukajifanya hadi kufuta namba kwenye simu yangu ili nisiwasiliana na huyo P” “Daaah kweli bro nilifanya kosa kubwa sana, sasa ikawaje mpaka unawasiliana na P kiasi hicho inamaana ameshakua demu wako?” “hahahaha hapana hajawa demu wangu, ila si unajua mwenyewe watoto wazuri wanavyopagawa na mimi? Wewe tatizo lako maneno mengi halafu unapingana na ukweli wa mama kwamba mimi Hb” “kwahiyo huo u Hb wako bro unataka unichukulie na mwanamke ambaye nataka kuoa kaka? “sikia mie sijamchukua ila mtoto amenikubali sana, kuna mbinu kubwa sana nilitumia hadi kumleta hapa home sasa nakupa masherti ukiyatimiza Prisca atakua wako” “mmhh kaka masharti gani hayo?” “cha kwanza nataka elfu hamsini yangu irudi fasta, cha pili nahitaji kumuona yule mwanamke uliyemtumia hela na suala la mwisho unatakiwa uachane na videmu vyako vyoote na uanze maisha mapya, uwe unaenda kanisani kumuomba mungu, na unatakiwa uwe unaijua bibilia..je upo tayari?” “bro elfu hamsini yako hata kesho naweza kukupa ila kumpata yule demu itakua ngumu kwasababu sikuhizi hata simu yangu hapokei, kuhusu kuachana na umalaya nitaacha kabisa kaka kwaajili ya Prisca” alisema Alvin huku akijifuta machozi “basi fanya niipate hela yangu kesho” BAADA YA ALVIN KURUDISHA HELA Nilimwambia nitamsaidia kumuunganisha na Prisca kisha mambo mengine atamaliza yeye mwenyewe, kila siku nilikua nikichat na Prisca huku nikimsifia sana Alvin kwa mambo mengi, wakati huo tayari nilikua nimeshaanza kusoma chuo pale Mlimani masomo ya sheria na Alvin alikua anasoma IFM alichukua uhasibu, Prisca alikua anakuja kunitembelea chuoni huku akijitahidi kuonyesha hisia zake kwangu, wakati huo mie nilikua nimeshaamua kumsaidia Alvin ili awe na Prisca…. Alvin alianza kubadirika kama tulivyokubaliana, alinionyesha moyo wa kuhitaji kuwa na Prisca kwasababu tulikua tunaenda kanisani pamoja na ule uhuni akawa ameuweka pembeni, kuna siku nilimtania “dogo kwanini usiachane na mipango ya kuwa na Prisca ukaishi maisha haya ya kumpendeza mungu?” “aaaahh bro unanibadirikia sasa, si tulikubaliana nifuate haya niwe na Prisca” “sijakubadirikia ila nakushauri tu” “bro mi nampenda Prisca na ninaomba mungu niache hata chata kwa Prisca” “chata ndo nini?” nilimuuliza Alvin “hahah I mean mtoto, lazima anizalie bwana” “wee wee si unajua yule mwanafunzi” “si akimaliza, mie nataka kuoa kabisa kaka” “mmmhh sawa dogo, kweli umeamua safari hii” Miezi ilizidi kukatika na mipango ikatimia hatimae Prisca alimuelewa Alvin na wakaanza mahusiano, Prisca kilichomfanya amkubali sana Alvin ni kwenye masomo ya hesabu alikua ni imara sana, na alikua akiamua kukufundisha basi lazima utaelewa tu hatakama uwe kichwa kigumu vipi… Prisca alimpenda Alvin na walishibana kisawasawa na maisha yalisonga kama kawa na hapo ndipo mapenzi yaliiva kwa hawa wawili wapendanao. BAADA YA KUMALIZA MASOMO Baada ya kumaliza degree ya sheria chuo kikuu Mlimani nilienda south Africa kuendelea na master ya sheria chuo kikuu cha South Africa na kumuacha Alvin akiwa tayari ameshaajiliwa Bandari kuu ya Tanzania(TPA) akiwa kama muhasibu pale… Nilitumia mwaka mmoja kumaliza master yangu ya sheria na niliporudi nyumbani nilikuta tayari Alvin anamaisha mazuri tu japo alipokua anataka kuhama nyumbani lakini wazazi walikua hawapo tayari kumruhusu ahame nyumbani hapo, Tuliendelea kuishi mikononi mwa wazazi huku Alvin akiendelea na kazi wakati huo mimi ndo nilikua bado sijapata ajira.. Wakati huo Prisca alikua bado yupo na Alvin kama kawaida kitu ambacho kilinifanya nifurahi sana n kuamini kwamba Alvin alikua anampenda sana Prisca na alikua na malengo naye, kipindi hicho Prisca alikua yupo form six,yaan alikua ni mdada mdada kweli, alikua anakuja mara nyingi sana kunisalimia na muda mwingine tulikua tunaenda out huku akinitania tania na kunieleza kwamba bado kuna kitu anahisi anaizulumu nafsi yake, nilijaribu kumuuliza akawa hasemi zaidi ya kuniambia “FOOT PRINT” “unamaanisha nini Prisca?” “Rudisha kumbukumbu zako miaka mitano iliyopita first time nilipokuja kwenu Calvin” Nilikua najaribu kurudisha kumbukumbu nyuma nikakumbuka kwamba hayo maandishi yalikua kwenye tshert ambayo nilikua nimempa mimi siku ile ya kwanza kuja home baada ya kumwagikiwa na juisi blauzi yake, nilitabasamu kisha nikamuangalia usoni naye huku akitabasamu na zile dimpoz kuzidi kuchukua nafasi usoni kwake… Akili yangu nikajua aliipenda sana ile tshert basi nikawa naishia kucheka tu na kumwambia asijali nitampa nyingine, Kuna siku nilikua nimeenda posta nikapita nje ya duka moja la nguo kule mitaa ya Samora ndipo nikaona mlangoni kuna tshet imeandikwa Foot Print nikaamua niinunue then nitampatia shemeji yangu kama zawadi, baada ya kununua siku ya siku Prisca alipita home kunisalimia ndipo nilipompa tena ile tshert na kumwambia zawadi ile asiitoe mle kwenye bahasha mpaka atakapofika kwao ndo aifungue, Prisca akanishukuru na kuondoka zake huku akiniacha nipo tu home, wakati huo nilikua bado sijaanza kazi Kuna ofisi binafsi za mawakili zipo pale mnazi mmoja nilijaribu kupeleka Cv zangu wakazipokea na hapakua na ubabaisho wowote ule nilikua tayari nimeshaanza kazi…. Nilichapa kazi kwa umakini sana na nilihakikisha kila kazi ambayo napewa basi namuomba mungu kwanza ndipo naifanya na ilikua lazima nifanikishe hata kama ilikua ngumu kiasi gani basi ikija mikononi mwangu tu basi sio ngumu tena, maisha yaliendelea vizuri na muda mwingi sana gari ya Alvin nilikua naitumia mimi ambayo ilikua inanirahisishia kwenda kazini… Kuna siku nikiwa ofisini iliingia text kutoka kwa Prisca iliyoandikwa “Foot Print” nilitabasamu tu kisha nikamwambia “nitakuletea tena nyingine mama” “sijamaanisha hivyo Calvie” “unamaanisha nini shemu wangu?” nilimuuliza Prisca “namaanisha…….” Text ndivyo ilivyoandikwa,kiukweli sikuelewa kabisa ikabidi nimtext tena “unamaanisha nini mbona sijaelewa P?” “Namaanisha Foot Print” Mmmhh Prisca aliniacha njia panda ikabidi niongee na mfanyakazi mwenzangu pale ofisini nimsimulie jinsi ilivyo mwanzo mwisho, na mara ya mwisho ndo nimekua nikipokea text za namna hii FOOT PRINT.. Jamaa alikua ameielewa vizuri ile text na akaniambia maana ya yule mwanamke ni kwamba anahitaji muhuri wako, FOOT PRINT inamaana kwamba ukikanyaga chini na unyayo basi lazima utaacha alama flani ya miguu, sasa na wewe unatakiwa uweke alama yako kwake ili ionyeshe kwamba ulipita, “Duuhh ndo anavyomaanisha?” nilimuuliza yule mfanyakazi mwenzangu “yap Mr Calvi huyu mwanamke ndo anavyomaanisha, inaonekana kuna kosa ambalo umelifanya kwake” “kosa?? Kosa gani tena Mr? “mie siwezi jua kwakweli, ila mara nyingi inatokea hivi kama mwanamke amekua akikupenda sana halafu ukazingua then akawa na mtu wa karibu yako so lazima hisia zake zitaendelea kubaki kwako kama bado mtakua mnaendelea kuonana”aliniambia yule wakili mwenzangu “mmmhh kaka sasa unafikiri nitafanyaje sasa hapa na ukicheki huyu binti anatembea na mdogo wangu kabisa” “Wanawake bwana sio wote ambao wanakua wanaupeo wa kufikiria mbali, kawaida wanakua wanataka lile jambo ambalo linawazwa kichwani mwake lazima litimie hhafikirii mbele kama kuna madhara au la. Cha msingi wewe muepuke kumweka karibu inaweza ikakusaidia Mr Calvin” “thanx kaka kwa ushauri” Baada ya kupata ushauri huo kutoka kwa Mr Cole ambaye nipo naye ofisini hapo ikanibidi nipunguze mawasiliano ya karibu na Happy na mwisho wa siku nikawa hata sipokei simu yake kwasababu niligundua yupo na Alvin kwakua tu mimi nilijitahidi kumshauri lakini kiukweli yule mwanamke alikua bado ananipenda sana… ******************* Foleni ni kubwa barabara ya morogoro road, Kwenye mataa magomen inakuja gari ndogo aina ya Ti nyeusi ikitokea ubungo na kuingia kwenye foleni hiyo, dereva wa gari hiyo aina ya benzi ni kijana mtanashati Calvin niliyevalia shati jeupe na tai nyeusi,,,nilikua naonekana nikiwa busy kuongea na simu, huku nikirekebisha tai yangu(ile tai ilikua imenibana sana pale shingoni).. Wakati huo pembeni kuna gari nyingine ndogo aina ya Alteza ambayo ndani ya ile gari kulikua na binti mzuri ambaye alikua akionekana akinywa kitu kwenye kikombe maalumu huku akiwa makini kuangalia taa zinavyopokezana kuongoza magari kwenye makutanano ya magari yatokayo ubungo, ilala, mikocheni na kariakoo…. Ile gari ya yule dada ilikua imekuja kusimama sambamba kabisa na Gari yangu niendeshayo ambayo ilikua ni ya Alvin.. Niliiangalia ile gari iliyokuja kusimama pembeni yangu ndipo nilipomuona mdada mzuri sana ambaye amekaa ndani ya ile gari akiwa bize akiendelea kunywa kinywaji chake Ghafla.. Mmoja ya watoto wanaoshinda barabarani anamwagia maji kioo cha mbele cha gari ya yule dada na kuanza kukisafisha Yule dada alipiga honi mfurulizo na kumzuia yule mtoto kwa kumuonyeshea ishara za mikono kwamba aache asioshe kile kioo,wakati huo alikua vioo vyote kavifunga anakula A/C tu mdada wa watu. Yule dogo aliacha kufuta lile gari,na kuvuka upande wapili kuendelea na shughuli yake, wakati huo yule dada alikua amewasha weper za gari yake na kusafisha kioo kile cha mbele ya gari lake Wakati huo mie nilikua busy nikiendelea kuongea na simu huku namtazama tu yule msichana kisha nikakata simu na kushusha kioo cha gari langu, nikapiga honi na kumuonyesha ishara kwa mikono yule dada kumuomba ashushe kioo niongee naye mara moja Yule dada akaacha kunywa kile kinywaji na kuniangalia kama hamuelewi vile nilivyokua nampa ile ishara,niliendelea kumuonyesha ishara kwamba ashushe ndipo akanielewa na kushusha kii chake, kwakua ile gari yake ilikua ni left hand basi haikua shida kuwa karibu na mimi kwasababu gari niliyokua naendesha ilikua ni light hand hivyo tukawa tupo karibu na ndipo nilipopata chance ya kumuongelesha “habari yako mrembo “(huku nikitabasamu) “safi tu…” alijibu yule dada huku akiniangalia kwa umakini ” samahani dada nina njaa sana hapa (huku nikishika tumbo langu) naomba na mimi nipate japo hata kidogo hicho unachokunywa wewe…” Wakati huo naongea hivyo nilikua anaongea nikiwa serious ”hahaa..you are so funny,,,this is one cup,one user,,utaweza kushea kikombe na mimi, harafu hata hujui nakunywa nini unaomba tu hee..” alisema yule mrembo huku akinishangaa ”usiwe mchoyo dada we nipe tu, najua kama wewe kinakufaa basi hata mimi kitanifaa pia, harafu kuhusu kikombe usijali nitashea tu” nilimwambia huku nikitengeneza sura ya amani na upendo usoni kwangu Yule dada alitoa kicheko na kukiinua kile kikombe juu kidogo na kukiangalia “hahaa hakika mimi si mchoyo lakini hii ni yangu na ni kwa ajili yangu tu..” ”ngoja nikuambie kitu.. miaka kadhaa iliyopita kulikuwa na watoto wawili wakicheza mpira lakini mmoja alikuwa kila mara akikataalia mpira wake akidai ni wake hatampa mtu kucheza,,,siku moja akiwa anacheza akapiga mpira ule ukaingia kwenye kidimbwi cha maji,,akamwambia mwenzake amsaidie kuutoa kwakuwa yeye ni mfupi hivyo akaogopa kuzama,,mwenzake akamkumbusha kuwa ule ni mpira wake peke yake na hivyo akaufate mwenyewe,,,(huku nikitabasamu)hiyo ni hadithi ya mwenye chake na majanga yake,,,so…unanipa ninywe au? halafu foleni ndo inaondoka ivyo,,” nilimwambia yule dada lakini maneno yangu yalionekana kumshinda yule dada “hahaa haya bwana umeshinda wewe..” alisema yule mrembo huku akinyoosha mkono na kunipatia kile kikombe “asante sana,,” nilimshukuru huku nikitabasamu na kunyoosha mkono kupokea kile kikombe,wakati huo foleni ikisogea taratibu huku watu walio kwenye magari mengine wakiangalia ule mchezo bila kujua nini kinafanyika pale, ghafla yule dada akaongea ” ooohh sorry,,,how can i get my cup back??”(samahani nitakipataje kikombe changu) Huku taratibu gari zikianza kutembea ”Tutaonana jioni saa 11 hivi au?” “okey,,,nadhani ni muda ambao na mimi natoka kwenye mishemishe zangu foleni inazidi kusonga mbele na hatimaye kila mmoja anakamata njia yake kuelekea kutafuta maisha…. ************* Jioni nilitoka mapema sana kazini ili saa 11 ikanikute nipo pale kwenye mataa ili niweze kuonana na yule dada ambaye tulipanga tuonane pale muda ule ili nikampe kikombe chake na nipate muda wa kuongeanaye vizuri, kutokana na jioni kunakua na foleni kubwa zaidi hata ya asubuhi nilijikuta saa kumi na moja ikinigongea nikiwa jangwani kwenye foleni huku manyunyu ya mvua yalikotokea sijui, niliilaani sana ile mvua pamoja na foleni, kwasababu tulikaa jangwa kama dakika arobaini hivi, hadi nafika kwenye mataa ya magomeni ilikua tayari ishafika saa kumi na mbili kasoro na sikuweza kumuona yule dada hivyo nikapita pale nikiwa nimenuna huku kichwani nikikumbua ile sauti yake ya upole na ukarimu, yaani kama nilikua namuona vile,nilikua natamani sana kumfahamu kiundani yule dada ambaye alikua namuonekana wa dada mchapa kazi hodari na mwenye kujua upendo, niliweza kuujua undani wa moyo wake kwa muda mchache tu ambao niliokua nimeongeanae, hiyo yote ni kutokana na kazi yangu niifanyayo na kukutana na watu wa kila aina katika maisha yangu… Niliingia home nikiwa nimechoka kutokana na msongamano wa foleni barabarani huku nikiwa bado namuwaza yule dada, nilitamani nimsimulie Alvin lakini nikaona bado mapema sana kumpa hizo taarifa hivyo nikapiga kimya na usiku ukachukua nafasi nikalala Sikuweza kuonana tena na yule mwanamke mpaka nilipokuja kukutana naye ilikua ni ofisini ambapo nafanyia kazi, najua unatamani ujue mpaka mwisho yaliyotokea juu ya huyu mwanamke, endelea kusoma utapata jibu ujue kilichojiri!! ***************************************** Kutotaka na ubusy wa kazi kuwa nyingi na pale majukumu yakaongezeka baada ya mimi kuanza kazi, kulikua hakuna mtu wa kumsaidia mama kazi ndogo ndogo za pale nyumbani hivyo mama akaona ni bora yule msichana wa kazi ambaye aliandaliwa na bibi toka kijijini kwetu aletwe mjini, mama alimpigia simu bibi kisha akatuma nauli kijijini na kuwafahamisha kwamba waende mjini wakamkatie tiketi yule binti tayari kwa kuja Dar…. Baada ya maandalizi kukamilika Somoe alisafirishwa kuja mjini Dar es salaam, mimi na Alvin ndo tuliyeenda kumpokea huyo binti, hakuwa na simu ila tulipewa maelekezo jinsi Somoe alivyovaa, Tulienda ubungo mapema sana kusubiria mabasi yatokayo Masasi, wakati tupo kituoni hapo kama kawaida yake Alvin hakuishiwa maneno ya kuongea “kaka huyu binti akiwa mzuri basi lazima nimpe dawa” “Alvin mdogo wangu hebu kuwa mstaarabu yaani mie nimejitahidi kukubadirisha nikakupa mtoto mzuri utulie lakini bado unamtaka hadi beki tatu??” “aaahh bro mie nataka nimzindue kabla wachizi wa mtaa hawajaanza kufanya yao” “ddaah we ndugu yangu ni hatari sana” “basi nikuachie wewe bro” “mie sitaki, tena huyu ni kama dada yetu sasa wewe ukileta habari zako itabidi nimwambie Prisca” “Duuhh yamekua hayo? Poa basi kaka nimekuelewa” Muda mchache baadae nikiwa bado napiga story na Alvin zilitawala kelele za honi huku na huko pale ubungo stendi ya mabasi ya mkoani, muda huo ndo basi za mkoani zilianza kuingia, hapo ikatubidi tuinuke pale tulipo tumekaa tukawa makini sana kuliangalia basi ambalo Somoe alikua amepanda “bro gari lenyewe hilo hapo linaingia” alisema Alvin, “yap sasa inabidi tuwe makini sana asije akapotea” Tulilifuata lile basi hadi mahali ambapo lilikua limeenda kusimama kisha tukaa pembeni tukitupia macho pale mlangoni, Abiria walikua wengi sana ambao walikua wanateremka lakini kuna mmoja ambaye alikua amevalia miwani aliteremka moja kwa moja mpaka nilipokua nimesimama mimi na Alvin kisha akaomba nimuonyeshe ambapo zinapark teksi kwasababu yeye ni mgeni na pia sio mwenyeji hapa Dar … Nilimwambia kama hana haraka asubirie kuna mgeni tunampokea halafu tutaenda wote hapo kwenye taksi, yule dada alikubali, tukiwa bado tunatupia macho pale mlangoni tuliweza kumuona somoe akiteremka kutoka ndani ya lile basi huku akiwa ameshika muhogo mkono wa kushoto huku mkono wa kulia kashikiria mfuko wa Rambo huku kwapani kwake akiwa amebana kopo la maji ambayo alikua amepewa mle ndani ya basi… Somoe alikua amevaa kibush bush kweli, alikua kava gauni la dukani lenye maua maua huku juu yake amevalia na khanga akiwa amejifunga lubega(alikua amejifunga shingoni ile khanga), kichwani alikua amesuka mtindo wa twende kilioni japokua hizo nywele kwambele zilikua zimefumuka fumuka, sikupata tabu kumjua Somoe hiyo yote ni kutokana na kupata maelekezo jinsi vile alivyokua amevaa, nilimfuata haraka haraka na kumpokea ule mfuko wake wakati huo Alvin nilikua nimemuacha amesimama na yule dada ambaye alikua anataka tumuonyeshe zilipopark tax, kimoyo moyo nilisema dada kuwa makini hapo nimekuacha na fisi Baada ya kumpokea ili mizigo yake tulielekea pale alipokua amekaa Alvin kisha tukajumuika pamoja na kutoka nje ambapo zina park tax, “oya bro muangalie dada yako” alisema Alvin huku akicheka, Niligeuka na kumuangalia Somoe ambaye alikua yupo kwa nyuma kidogo, nilitamani kucheka ila nilijizuia nilihisi angejisikia vibaya…. Somoe alikua akishangaa shangaa huku na huko huku akila ule muogo mbichi ambao alikua ameushika mkononi huku akishushia na maji yake, alikua akipigana vikumbo na watu kila baada ya sekunde kadhaa hiyo yote ni kutokana na ushamba wa kushangaa aliokuanao Somoe…. Ilinibidi nisimame kumsubiri asogee karibu kisha nikamshika mkono, tuliposogea karibu na ile tax yule dada tuliagana naye pale huku tukitambulishana majina, ila chaajabu ambacho kilinishangaza ni kwanini Alvin alikua mpole sana na hakuweza hata kusema neno lolote lile kuhusiana na yule dada aliyekua amevalia miwani nyeusi, tishert ya njano na jinsi nyeusi, Yule dada baada ya kuondoka sie tukachukua tax, Alvin alikimbilia kukaa mbele kisha nyuma tulikaa mimi na Somoe,ngoja nikupe umbea kidogo ila usimwambie na mwenzio sawa?? Ni hivi ile khanga ambayo alikua amevalia Somoe kwa juu ilimfunuka wakati anainama na kuingia kwenye tax hivyo niliweza kuona vilivyo huku nyuma kwake, kumbe ile khanga alijifunga vile ili kuziba tobo ambalo lilikua lipo kwenye lile gauni lake huku nyuma, hapo ndipo nilipopata jibu ambalo nilikua najiuliza kwanini kava gauni zuri halafu kafunga khanga kwajuu, pia ile khanga ilikua na maneno ambayo yalikua yanasomeka hivi “MTANIKOMA” Siku yatilia maanani sana yale maneno ambayo yalikua yameandikwa kwenye ile khanga kumbe yalikua yamebeba ujumbe mzito sana, Muonekano wa Somoe ulikua ni mzuri sana, alikua anaonekana ni mwanamke ambaye akioga maji ya chumvi ya mjini Dar es salaam siku kadhaa tu atabadirika, Basi tukaanza safari ya kwenda home na tulipofika home mama alimuonyesha chumba cha kulala kisha akampa maneno machache ambayo ni “ hapa nyumbani hautoishi kama house girl, utaishi kama ndugu wa hii Familiaya Ambonile, huyo hapo ni Calvin utamueshimu kama kaka yako na yule pale anayekunywa maji kwenye friji anaitwa Alvin ni mdogo wake Calvin,naye utamuheshimu kama kaka yako” Mama alimpa maelekezo machache jinsi ya kuishi pale nyumbani kisha shughuli nyingine zikaendelea kama kawaida BAADA YA MIEZI KADHAA KUPITA Nilikua busy sana na kazi kwenye ofisi ya kujitegemea ambayo ni maarufu sana mjini hapa Dar es salaam ambayo ilikua inaitwa MKOMBOZI WAKO, nilikua nikitoka nyumbani asubuhi na kurudi jioni, nilikua mchapa kazi mzuri sana kazini hapo, kesi nyingi za watu nilikua nikikabidhiwa na nilikua nazifanya vizuri sana na kuhakikisha lazima tunashinda hizo kesi…. Niliongezewa mshahara kazini huku kampuni binafsi zilikua zikinihitaji na kunitangazia mshahara mnono sana, kikubwa kilichokua kinanipa nguvu na kunifanya nifanye vizuri sana katika kazi zangu nikutokana na kumtanguliza mungu mbele huku nikiyapiga teke mapenzi, sikutaka kabisa kuyashirikisha mapenzi katika kazi zangu hicho ndo kitu pekee kilichokua kikinipa nguvu ya kufanya kazi…. Alvin naye alikua mchapa kazi mzuri sana kazini kwao japokua muda mwingi alikua akitumia muda mwingi kufanya starehe na watoto wa shule, alikua akikutana na mwanafunzi yeyote yule wa sekondari basi alikua anahakikisha atatumia gharama kubwa sana kuhakikisha anamtia mikononi…..hayo ndo yalikua maisha ya kila siku ya Alvin ambaye alikua ni muhasibu wa KONAMIC COMPANY UPANDE WA HOUSE GIRL Alikua mchapa kazi mzuri sana lakini miezi miwili baadae Somoe alibadirika kabisa, hakuwa Somoe yule ambaye namjua mimi na wewe, Somoe alikua tayari ameshatekwa na jiji hili la Dar es salaam, Taratibu alikua ameshaanza vitimbwi, tabia ilianza kumbadirika, alianza kubana bajeti kwa kila hela ambayo ilikua inaachwa nyumbani pale kwaajili ya matumizi, kila siku alikua anapika maharage huku hela akizibania na kwenda salun kuseti nywele zake, nilijaribu kumuuliza kinachomfanya apike maharage kila siku basi alikua haishi cha kujitetea…. Kwakua nilikua sio muongeaji sana hivyo suala lile nilikua namuachia mama alifuatilie ila mama alionekana kama kumshindwa Somoe, na mbaya zaidi ni pindi tu pale tulipokua tumemnunulia simu kwaajili ya matumizi ya pale nyumbani basi kila mwanaume pale mtaani alikua na namba ya Somoe, muda mwingine Somoe alikua akienda sokono basi alikua anajipamba haielezeki, nilikua namshangaa sana kwa jinsi alivyokua ameanza kubadirika… Kikubwa kilichokua kimenijenga kichwani ni kwamba huenda labda anaenda na wakati si unajua maisha ya dar e s salaam, basi baada ya siku kadhaa mbele Somoe alikua tayari ameshashuka thamani pale mtaani na mbaya zaidi alipewa hadi jina “MAHARAGE YA MBEYA MAJI MARA MOJA” wengine wakamwita mchezaji hodari number One wa mtaa, yeye anacheza mchangani,vichakani hata kwenye majumba mabovu wala hajari hilo suala… Ikafikia hatua hadi mlevi wa zile pombe za bei rahisi,gongo,matapu tapu walikua wanamchukua Somoe, nilijaribu kumuita siku moja Somoe na kuongea naye alikosa cha kusema zaidi ya kulia na kusema wanamsingizia tu sio kweli, aliniomba nimsamehe na nisimfikishie mama hizo habari… Nilitamani sana kumwambia mama lakini nilikua nashindwa kwasababu nilikua najua kwamba somoe kaja mjini kutafuta maisha, hizo ni hulka tu ipo siku atatulia Somoe alizidi kubadirika ilifikia wakati nikirudi kutoka kazini basi alikua anakuja chumbani kwangu na kuanza kuniletea visa, nilikua najua ni nini alichokua anataka lakini kutokana na heshima kubwa niliyonayo nikaona ndo wakati muafa wa kumweleza mama na ikibidi Somoe aondoke nyumbani hapo, Mama alinisikiliza kwa umakini yote niliyomueleza akasema kwamba nay eye hizo habari anazo alikua anatafuta tu siku anifikishie, mie nikamuita Somoe kisha tukampigia mahesabu kwa miezi yote ambayo alikua amekaa nyumbani hapo kisha tukamlipa pesa yake na kumfukuza kabisa… Kitendo cha kumfukuza Somoe nyumbani hapo kilimuuma sana, hatukujua baada ya kumpa zile hela alienda wapi lakini nilianza kusikia tetesi mtaani kwamba Somoe anajiuza mitaa ya sinza na ameshanitangazia kila mitaa kwamba mie ni joka lakibisa, nilishangaa sana yale maneno ya watu ambayo yalikua yanasambaa mtaani ila kwakua nilikua najijua kwamba sina hayo matatizo niliamua kuachana na hizo habari huku nikiendelea kuchapa kazi kama kawaida MWEZI MMOJA BAADAE Nikiwa natoka ofisini ili nikapate lunch nikaona viatu vyangu vina vumbi hivyo nikaona ni bora nivipeleke kwenye kibanda cha shoe shine ambayo kipo nje ya ofisi yetu, nilienda pale huku nikimtania yule babu ambaye anafanya kazi ya kushona viatu na kupiga kiwi “babu leo nataka ung`alishe kiatu changu mpaka nijione” “hahahha babu haina shida kabisa hizi ndo kazi zangu babu” “haya babu ning`alishie hiki fasta nataka nikale babu” “sawa babu lakini kuna mzigo wako hapa nimeletewa na kijana mmoja niliambiwa ukitoka tu ofisini nikupe” alisema yule fundi viatu “mzigo gani babu” nilimuuliza huku nikipokea ile bahasha kubwa ya kaki Niliifungua kisha nikakutana na Gazeti moja maarufu ambalo lilikua limeandika kwa herufi kubwa “WEWE WAKILI UMAARUFU WAKO NI BURE IKIWA UNA MATATIZO YA UZAZI” Nilishtuka sana kukutana na zile taarifa, nililifungua ndani na kwenda moja kwa moja kwenye ukurasa ambao ulikua umebeba ile habari, ilikua imeenza na kusema …Wakili maarufu mjini Dar es saalam, ambaye anaongoza kwa kushinda kesi zote ambazo anakabidhiwa azisimamie amegundulika ana matatizo ya uzazi, hiyo hali imemuanza toka awe na miaka 16 na mpaka sasa, je unadhani anayafurahia maisha yake? Ni habari za ukweli na zenye kuthibishwa na mkazi mmoja ambaye anaishi Tandaele kwa mtogole lakini ni mfanya biashara mitaa ya sinza….. Nilishindwa kuendelea kwasababu nilijua wazi zile habari Somoe ndo aliyezipereka kwa waandishi wa habari, nikamuangalia yule babu na kumuuliza “unamfahamu aliyeleta hili gazeti?” “hapana babu simfahamu, kwani limeandikwa nini?” Sikumjibu yule babu niliinuka pale kwenye benchi ambalo nilikua nimekaa kisha nikaingia ofisini huku nikiwa nimevaa ndala tu wakati huo viatu vyangu vikiwa bado vinang`alishwa na yule babu… Nilitoka ofisini kisha nikarudi kwa fundi viatu nikachukua viatu vyangu nikavivaa kisha nikaenda moja kwa moja kwenye gari yangu na kuliwasha safari ya kwanza ilikua ni Sinza maeneo ambayo niliwahi kusikia Somoe anapatikana, nilipofika mtaani hapo nikaambiwa Somoe anaumwa sana amelazwa hosptali ya AMANA iliyopo ilala, Nilimchukua rafiki yake kwenye gari yangu kisha akanipereka hadi hosptali hapo ambapo sikuamini macho yangu, kwanza alikua amelazwa chumba cha peke yake.niliposogea karibu Somoe alikua ametumbua macho huku lile shepu alilokua anajidai nalo halipo tena, Somoe alikua amekonda kama njiti ya kiberiti, Somoe alikua ametoka vidonda mwili mzima, uso wake wote ulikua umepauka huku umeambatana na vidotidoti utadhani vijana wa vijiweni walikua wanazimia vishungi vya bangi au sigara zao kwenye mwili wa Somoe…… Nilitamani kumuongelesha lakini nilizuiwa na nesi ambaye alikua amesimama pembeni… Nilikua mpole sikuweza kuongea lolote zaidi ya kuishia kumuangalia tu pale, “huyo ndo Somoe unayemtafuta?” “aliniuliza yule dada ambaye nilikua nimeendanaye pale hospital” “mmhh hebu njoo tuongee mara moja…” nilimshika mkono yule dada kisha tukatoka nje na kuanza kuongea.. Yule dada aliniambia kwamba “Somoe amesumbuliwa sana na ugonjwa hatari wa Ukimwi, ugonjwa huo haufahamiki kapewa na nani ila aliorodhesha majina ya watu wengi sana ambao alitembeanao” “hayo majina yako wapi?” “hayo majina aliyaorodhesha alipokua anahojiwa na muandishi wa habari ambaye alitembelea hosptalini hapa kuona wagonjwa, kwahiyo Somoe akamuomba amuandikie habari yake fupi ambayo itakua funzo kwa wengine” “mmmhh okey asante dada kwa machache hayo yanatosha,” Niliinuka na kwenda kwenye gari yangu nikatoa lile gazeti ili nione majina yale huenda Alvin naye yupo” Niliangalia mwanzo mpaka mwisho sikuliona jina la Alvin, sikuamini macho yangu hivyo nilifurahi kuona mdogo wangu hayupo kwenye janga hilo maana hajui kabisa kutumia kinga yule dogo, Niliondoka pale hosptali huku Somoe wakimfanyia mpango wa kumsafirisha kwao, nilirudi kazini kisha nikaomba ruhusu ya kurudi nyumbani ili nikapumzishe akili yangu na kutafakari yale yaliyoandikwa kwenye gazeti lile la Udaku, Nilipofika home mama alishangaa kuniona nimerudi mapema nyumbani wakati ilikua sio kawaida yangu, sikutaka hata kuongea naye niliingia chumbani na kuanza kulisoma tena lile gazeti, Oooohh my God baba yangu alikuwepo katika orodha ya wanaume ambao Somoe ametembeanaome, iliandikwa hivi “baada ya kubobea katika shughuli hii ya umalaya wa kujiuza kimya kimya bosi wangu ambaye ndo nilikua naishi kwake alinitongoza na aliniahidi kuishi kifahari hapo nyumbani kwake hivyo sikuweza kumkatalia nikampa mzigo japokua sikumpenda kabisa, baada ya wiki mbili mbele mwanae ambaye ni mcheshi mcheshi na ni handsome kweli naye akaingia kwenye line zangu naye nikampa mzigo…. Swali la kizushi kutoka kwa muandishi: ulivyokua unalalanao kuna ambaye alikumbuka kutumia kinga kati ya huyo mzee na mwanae?” Somoe: huyu bosi wangu mwanzoni alikua anatumia ila baada ya kulala naye kama mara tatu hivi akaacha kutumia tukawa tunafanya kavu kavu Mwandishi: hahahaha na huyu handsome boy. je? Kwani jina lake nani?” Somoe: huyu hajawahi kutumia hata mara moja…jina lake siwezi kutaja ila limeanza na A…. Mwandishi: vipi huyo mwanasheria ambaye ni mtu wa mungu sana hakuwahi kuingia hata kidogo kwenye 18 zako??” Somoe: aaahh mkali huyooo si unajua wanasheria walivyo? ila nilikua namvizia na yeye nimpe hata mara moja lakini nilimkosa….. Nilihisi kuchanganyikiwa na nikagundua kwamba nilipokua kule hosptali nililisoma gazeti hili kwa haraka sana kwasababu presha ilikua imeshanipanda juu, Nilivuta picha ya nyuma kidogo nakugundua kwamba kwanini baba alikua akimtetea sana Somoe pindi alipokua akifanya kosa pale nyumbani, Baba alikua hapendi kuona tukimfokea Somoe huku akisema bado hajazoe mji,alitaka Somoe aishi free na afanye anavyotaka kumbe alikua ni mke wa pili wa baba yetu mle ndani bila sie kujua, hapo ndipo picha kamili iliponijia na kukumbuka ile siku ambayo baba aliondoka na Somoe isijulikane walienda wapi na wakachelewa kurudi kumbe walikua wameenda kufanya ufuska wao Kwakua baba yetu alikua anaonekana mpole hakuna hata mmoja pale nyumbani angefikiria kama baba angekua natabia ile ya ushenzi kutembea na mfanyakazi wa ndani huku akila sahani moja na mwanae, Kumbukumbu zilinijia na kukumbuka kwanini baba alikua anamchukia sana Alvin, kwanini baba alikua hapendi kumuona Alvin akikaa na kuongea na Somoe, hapo nilikumbuka kwanini baba alikubali kwa ulahisi sana alvin akaishi maisha ya kupanga ili ajitegemee huku mimi akinizuia nisitoke nyumbani hapo..machozi yalinilenga usoni yakanichuluzika huku nikijiaribu kuyazuia kwa mkono lakini yalipata nafasi na kudondokea kwenye gazeti pale ambapo palikua pameandikwa “aaahh mkali huyooo si unajua wanasheria walivyo? ila nilikua namvizia na yeye nimpe hata mara moja lakini nilimkosa….. Nilianza kujengwa na roho ya kikatili ndani ya moyo wangu zidi ya baba yangu, nilitoka mle chumbani kisha nikaenda nje bila hata kujielewa naenda wapi, nilipofika nje hata sikukaa nikarudi tena chumbani huku nikipishana na mama pale ukumbini… Niliingia chumbani nikampigia simu Alvin an kumuomba tuonane, Alvin alikubali lakini aliniambia akitoka kazini ndo atanitafuta, sikukubaliana na maneno ya Alvin niliwasha gari na kumfuata kazini kwake, Ile naingia kwenye geti la kuingilia ofisini kwa Alvin nilimuona kwa mbali akiwa amesimama na mwanafunzi huku akimuhesabia hela kutoka kwenye wallet na kumpa yule binti, nilisikitika sana kuona ile hali niliamini tayari yule mwanafunzi ameshaharibiwa ndoto zake kwasababu Alvin ni muhasirika sasa… Nilipark gari langu kisha nikateremka haraka haraka, Alvin aliponiona nimeingia na gari yangu akamwambia yule mwanafunzi aondoke fasta kwasababu anajua lazima ningemuwakia… “Alvin hujaachana kabisa na hawa watoto wa shule?...hebu soma hili gazeti ukurasa wa nane” “kaka hata salamu hakuna?” “salamu haina umuhimu kama hili gazeti” “mmmhh kuna nini tena” Alvin alipokea lile gazeti kisha akavaa miwani yake na kuanza kupitisha macho kwenye lile gazeti, “whaaaaat Somoe kafanyaje….?”aliniuliza Alvin ila sikumjibu na mimi nikamtwanga swali “ushamaliza?” “oooohh no I cant believe” “ndo uamini, sahizi nimetoka hosptali Somoe yupo hoi bin taaban na huo ndo upuuzi ambao ulikua unawafanya mchukiane wewe na baba” “inamaana Somoe alitembeana baba?” “hilo sio swali Alvin hilo ni jibu, harafu kila siku nilikua nakushauri upunguze tama ya wanawake ulikua unielewi, sikia naenda home ukitoka job nitafute” Nilimwambia Alvin huku lile gazeti nikiwa nimemuachia mkononi akiwa amesimama amepigwa na bubuwazi… Niliingia ndani ya gari langu nikawasha na kuingia barabarani kuelekea nyumbani, njiani nilikua nawaza endapo baba akizipata taarifa hizi atazipokeaje? Mzee anasumbuliwa na presha ambayo iliambatana na ugonjwa wa kisukari, nilitamani ningezipata taarifa hizi mapema ili ningeweza kwenda kiwanda cha gazeti hili la UKWELI WA LEO (Jina la gazeti)nikapata kuongea nao na kuingia gharama zozote zile ambazo wangelizihitaji ningelipa ili kuzuia hii habari isichapishwe Gazetini.. Siku hiyo haikuwa nzuri kwangu, muda wote nilikua na mawazo tu, nilianza kumfikiria mama yetu ambaye alikua anatupenda sana, nilikua nafikiria mama atakapokuja kujua ukweli kuhusu baba alivyotembea na Somoe kutakua na Amani kweli? Magazeti tayari yameshaingia mtaani, nahisi heshima ya familia yetu itapungua, nilianza kuwaza kwanini somoe kanichafua kiasi kile na kuiharibu familia yetu…. SIKU NNE MBELE (Calvin anaendelea kusimulia) Nikiwa kazini kazi zilikua haziendi vizuri japokua nilitoka kuongezewa mshahara jana yake baada ya kuisimamia kesi moja ya mtu maarufu sana serikalini na kushinda ile kesi, ofisi iliniongezea mshahara nusu ya mshahara ambao nalipwa… Utendaji wa kazi siku hiyo ulishuka kiwango kutokana tu na mawazo ambayo yaliniandama, nikiwa kazini nasinzia nilipigiwa simu na Alvin lakini sikuona umuhimu wa kupokea simu yake nikakata simu yake, muda mchache baadae nikapigiwa tena simu kwa namba ngeni lakini nayo sikuipokea ndo kwanza nikaamua kuzima simu yangu, “ngrii ngrii ngrriii” Simu ya mezani iliita zaidi ya mara tatu bila kupokelewa,muda huo nilikua nimelala na mlio wa simu nilikua nausikia kwambali sana, mlango wa ofisini kwangu ulifunguliwa kisha simu ikapokelewa, aliyeingia na kwenda kupokea simu yangu ya ofisini alikua ni Secretary wangu na jibu alilowapa “kuna lolote la kiofisi naweza kukusaidia” “mie ni mama yake na Calvin na ninashida ya kuongea na mwanangu” “Mama anataka kuongea na ww” alitamka secretary wangu baada ya kuniamsha pale nilipokua nimejilaza” Niliamka na kuongea na mama, sauti ya mama haikuwa ya kawaida alikua akiongea huku akiambatanisha na kilio, “mama kuna tatizo gani?” “Calvi…baba…baba…baba yako..” “baba kafanyaje tena?” “baba ya….ba….baba yako…” Kabla mama hajamaliza kuongea simu ilikatatika, niliinuka haraka haraka huku nikisahau ufunguo wa gari pale ofisini juu ya meza kisha nikatoka mbio kutoka nje kuelekea parking ya magari, nilipofika hapo nje ndipo nikagundua kwamba ufunguo wa gari nimeusahau ndani hivyo nikarudi tena ndani kuchukua funguo za gari kisha nikawasha gari na kuchoma mafuta kuelekea nyumbani….. Kabla sijaikaribia nyumba ya Mzee Ambonile ambapo ndo nyumbani niliona mkusanyiko wa watu na magari yakiwa nje ya nyumba yetu, nilihisi hakuna amani tena pale nyumbani, nilisogea na kuegesha gari yangu pembeni ya gari la Alvin kisha nikaingia ndani, mama aliponiona mimi alizidi kulia zaidi ya vile nilivyomkuta “mwanangu kila nikunapo namuona baba yako” alitamka mama huku akizidi kulia, hapo ndipo nilipopata picha kwamba baba kafariki Dunia, Nilitokwa na machozi na muda mchache baadae nilikuja kuchukuliwa na mzee mmoja na kuniambia mdogo wako yupo huku twende, nilienda kwenye hicho chumba ambacho alikua Alvin sikumkuta katika hali ya kawaida, Alvin alikua amezimia wamemvua shati wakimpepea, kilio na maumivu yalizidi kutawala ndani ya moyo wangu ila niliikumbuka biblia ambavyo inasema “anayecheka leo atalia kesho, na kila nafsi itaonja umauti” hivyo nikajipa nguvu na kujikaza japo nilikua naumia moyoni… Kuna watu ambao waliniambia baba yangu kafa kwa presha , kutokana na ugonjwa wake wa kisukari kumsumbua sana toka asubuhi huku wakijifanya kunificha ukweli ambao mie nilikua naujua mwanzo hadi mwisho, Mipango ya mazishi iliandaliwa na hadi kufika jioni mida ya saa kumi namoja watu tulikua tayari kwenda kumzika baba… Hadi muda wa kwenda kumlaza baba mahali pema peponi Alvin alikua bado hajapata fahamu na tayari alikua ameshapelekwa hosptali, tulienda makaburini kumzika Mzee Ambonile, ilifika wakati wa kushika chepe ili nitie mchanga ndani ya kaburi,niliposhika chepe tu iliingia meseji kwenye simu yangu lakini sikutaka kuisoma muda ule, nilitia mchanga na baada ya kumaliza maziko ya baba ndipo nikashika simu ili nisome meseji “ Somoe aliyekua mfanyakazi wenu alifariki jana usiku ila kazikwa leo saa nne asubuhi” Ile namba ilikua ngeni kwangu hivyo hata sikutaka kuhangaika nayo zaidi ya kusema “Alazwe mahali pema peponi” kisha nikaifuta meseji na taratibu safari ya nyumbani ilichukua nafasi Tulipofika nyumbani tulimkuta Alvin kalala ukumbini huku akiwa ameweka chupa kubwa ya maji ya Kilimanjaro pembeni, aliniangalia usoni machozi yakaanza kumtoka lakini nilimsogelea kisha nikamfuta kwa leso yangu huku nikimwambia “jikaze Alvin wewe mtoto wa kiume” nilimnyoshea mkono kisha tukashikanisha mikono, nikamuinua pale chini na kutoka naye nje tukaenda kukaa kwenye gari yangu huku tukijadili mambo machache… BAADA YA MWEZI MMOJA KUPITA Mimi na Alvin tulikua tumeenda Makaburini kufagilia kaburi la baba yetu kwasababu kesho yake ndo ilikua arobaini yam zee Ambonile toka afariki dunia, tukiwa makabirini hapo huku tumevalia nguo nyeusi na miwani nyeusi ilikuja gari aina ya Toyota Surf na wakateremka vijana wawili ambao walikua warefu, walikuja mpaka pale tulipokua mimi na Alvin kisha mmoja wao akasema “mambo Alvin” Alvin aliitikia salamu kisha wakanigeukia mimi na kuniambia samahani japo tunafahamu wewe ni mwanasheria mkubwa sana mimi ni police mpelelezi naitwa James na huyu anaitwa Massud huku wakitoa vitambulisho vyao vya upolisi na kummwambia Alvin upo chini ya Ulinzi huku wakimuomba mikono wamfunge pingu “hey nimefanya nini tena?” “utajua huko huko police” “noo hamnipereki bila kuniambia kosa” “Alvin nenda usibishane nayo nipo kukusaidia” nilimwambia Alvin wakamchukua na kuondokanae huku wakiniambia kituo cha polisi ambacho wanampereka Baada ya wao kuondoka mie niliondoka pale makaburini na kuelekea nyumbani kumpa mama taarifa juu ya yote ambayo yamempata Alvin, kwakua mama alikua ananiamini sana kwa kazi yangu ya uanasheria hivyo hakuwa na wasiwasi juu ya hilo aliamini muda mchache tu Alvin atarudi nyumbani… *************** Niliondoka na kwenda kufuatilia kosa ambalo Alvin alikua amefanya ndipo nilipokutana na majanga kituoni hapo…Alvin alikua na kesi ya kumtorosha mwanafunzi shule na kuishinae nyumbani kwake kama mke wake kwa muda wa miezi mitatu mototo haonekani nyumbani wala shuleni, Alvin anakesi ya kumpa mamba mwanafunzi huyo huyo ambaye alimtoa shule na kumfungia nyumbani kwake, Alvin amepewa kesi ya kumuharibia mwanafunzi masomo yake na kupoteza Ada za wazazi ambazo walikua wanamlipia huyo mwanafunzi…. Niliishiwa nguvu kabisa na nilishindwa nianzie wapi kumtetea Alvin kutokana na kesi yake jinsi ilivyo kwasababu ni wazi kabisa inaonyesha hatutaweza kushinda kutokana na sheria ambazo zimewekwa na rais wetu juu ya wanafunzi… Ilinibidi niombe kukutana na huyo Mwanafunzi na wazazi wake ili tupate kuongea machache ambayo yanaweza kuwasaidia wao na sisi pia, hapo ndipo aibu iliponijaa usoni Mzazi wa huyo mwanamke ni Mzee Mwaipoje ambaye nilishawahi kumshinda kwenye kesi yake moja hivi ambayo nilipewa nisimamie na tukamshinda yule mzee japo alitumia pesa nyingi sana pia alidiriki kunipa rushwa ili niiachie ile kesi aiendeshe wakili mwingine ila nilimkatalia, hapo ndipo nikaona mdogo wangu Alvin anaenda kuozea jela… Muda mchache tukiwa kituoni hapo kwenye chumba cha upelelezi polisi mmoja alitumwa aletwe huyo mwanafunzi ndipo alipoingia binti ambaye sikuamini macho yangu, Alikua ni prisca huku ameshikilia tumbo lake na mkono wa kushoto anatafuna karoti… Niliona aibu nikainama chini bila kusema chochote, mikono ilitetemeka huku jasho likinitoka kwenye vidole vya mikono “kijana unataka uzungumze nini na mimi?”aliniuliza baba yake Prisca Nilikosa chakuongea kwasababu yule binti namfahamu na nilikua najua wazi kabisa anamahusiano na Alvin ila nilikua sijui kama ni mwanafunzi “ulikua unasoma form ngapi?” nilimuuliza prisca “form Five kaka Calvie” “wee unamfahamu huyu?” Aliuliza mmoja wa polisi “ndio namfahamu kaka yake na Alvin.. Tuliongea mengi sana rakini hakuna hata moja tuiloelewana na mwisho wa siku tuliamua tu kesi ifikishwe mahakamani kutokana na kutofika muafaka SIKU YA KESI Wakili ambaye alikua anasimamia ile kesi ni Rolyn mwanamke ambaye nilikua nampenda sana muda mrefu, nilishawahi kujaribu kufanya mipango mingi ili nikahakishe nitampaje nilishindwa, huyu Rolyn nilishawahi kuwa naye Ofisi moja ya Mawakili wa kujitegemea na alishawahi kunishtaki kwa bosi wangu kwamba namsumbua sana pale ofisini na huyo bosi akaamua kuniita na kunionya juu ya hilo suala, Kwakua nilikua na True feelings of love nilijikuta nashindwa kuvumilia juu ya upendo niliokua nao kwa huyo Rolyn ambaye aliletwa ofisini hapo ili kuongeza nguvu ya kuwa na mawakili ambao wachapa kazi hodari…. Niliendelea kumsumbua Rolyn kwamba nahitaji kumuoa lakini haikuwa hivyo kama nilivyotegemea mwisho wa siku nilisimamishwa kazi kwa muda wa mwezi mzima ndipo nikaona nisirudi tena pale ofisini na kupata Ofisi nyingine ambayo nafanyanayo kazi mpaka sasa, kiukweli nilimpenda Rolyn na bado ananafasi kubwa ndani ya moyo wangu, ni mwanamke ambaye ameiweza akili yangu na kunifanya nianze kumpenda zaidi ya vile mwanzo….(ni short story kuhusu Rolyn) Sheria inasema mwanasheria wa upande mmoja (mshtaki) akihisi anahisia za kimapenzi na mwanasheria wa upande wa pili(mtuhumiwa) anaruhusiwa kuhailisha kesi na akatafuta wakili mwingi, hivyo ndo ilivyokua kwaupande wangu kwamba nilikua nampenda Rolyn zaidi ya maelezo, na kuna muda Alvin aliniita na kuninong`oneza “kaka huyo wakili si ndo yule aliyekusababishia uachishwe kazi pale WAKILI KWANZA?” “Yap ndo yeye umemkumbuka eeh?” “ndio kaka, sasa unauhakika tutamshinda kweli maana uliniambia yupo fit na anaijua sana sheria” “usijali Alvin kesi tutashinda” nilimjibu Alvin kisha nikarudi kuketi nilipokuanimekaa Alvin alikua pale kizimbani upande wa kushoto wakati huo upande wa kulia alipanda Prisca huku akiwa anakula karoti kama kawaida yake na mkono mwingine akiwa ameshika kopo dogo la chupo ya uhai kwaajili ya kutemea mate… Hakimu alikua tayari na muda mchache baadae kesi ilianza kusomwa, wakati kesi ikisomwa mie macho yangu yalikua kwa Rolyn tu, nilikua nashangaa jinsi mungu alivyomuumba mwanamke yule, Rolyn naye alikua akiniangalia kidogo kisha anaangalia pembeni, muda mchache baadae nilimuona mama yangu akiwa amekaa pembeni huku akionekana akitetemeka mikono huku akiwa ameiweka kama akiomba dua…. Kesi ilisomwa na muda wa utetezi ulipofika nilisimama nikasogea mbele, na kwenda kumuuliza swali Prisca lakini wakati namuuliza swali prisca akili yote ilikua ikumuwaza Rolyn hivyo nikajikuta nimeuliza swali ambalo lilikua halina point…. Hakuna hata mmoja pale mahakamani angetegemea kwa umaarufu wangu wa kushinda kesi ngumu ningeuliza swali lakijinga kiasi kwamba akimu aligonga nyundo na kumhukumu Alvin miaka 30 jela kwa kosa la kumtia mimba mwanafunzi na kumharibia masomo yake, hukumu hiyo iliambatana na faini laki tano….. Alvin alidondoka pale kizimbani baada ya kusikia hivyo na pia mama pale alipokua amekaa aliishiwa nguvu na kudondoka papohapo, Kwajinsi alivyokua akikazana kumuoma mungu hakutegemea kabisa kusikia yale kutoka kwa hakimu na hakuamini kama ningeshindwa kumtetea mdogo wangu!! Zilikuja ambulance zikawapakia mama na Alvin huku wakiwa wameambatana na polisi wane wenye bunduki na kuwapeleka hosptali… Mama yangu alipoteza maisha kwa mshtuko alioupata pale, na Alvin alipata fahamu masaa machache mbele na moja kwa moja akapelekwa jela huko mwanza gereza la sengerema…. Prisca naye alijifungua watoto mapacha ambao walipewa majina ya Samsoni na Samweli, watoto hao walilelewa na bibi tu ambaye ni mama yake Prisca wakisaidiwa na msaada wangu, Najua utatamani ujue kwanini walilelewa na bibi tu, Prisca baada ya kujifungua alifariki ndani ya wiki moja.. Kilichomuua ni kwamba aliambiwa asiwanyonyeshe watoto hao kutokana nayeye alikua ni muathirika wa ugonjwa wa ukimwi, Aliyempa ugonjwa huo mimi sijui japo Alvin alishatembea na Somoe ambaye naye ametangulia mbele ya haki kwa gonjwa hilo hilo hatari la ukimwi… Baada ya Prisca kuambiwa hivyo aliamua bora tu afe hakuona umuhimu wa kuendelea kuishi duniani, Jaribu kuvupa picha kama ningeweza kutimiza lile neno la FOOT PRINT ningekuwepo wapi sahizi?? Afya yangu ingesomaje? “Duuhh baba na wewe si ungekuanao” “ni kweli ningekuanao, ningehangaika kama anavyoangaikanao baba yenu huko jela” “Hee kwahiyo baba yetu yupo jela na ana ukimwi?” aliuliza mtoto mmoja kati ya wale watoto mapacha aliozaa Prisca ambao ndo nawasimulia hii story “ndio Samweli, baba yako mzazi yupo jela, mimi ni baba yako mkubwa” “atatoka lini sasa?” “muda sio mrefu atatoka hata msijali” “kwahiyo baba wewe demu wako yuko wapi?” aliniuliza Samsoni “hahahah wanangu msijali muda sio mrefu nitawaonyesha mama yenu sawa eeeehh?” “Sawa baba” waliitikia watoto wale watoto huku mmoja akisema “baba mie basi nitakua naitwa jina lako kuanzia leo mie nitakua Calvin na huyu atakuwa Alvin” “awe mie nitakua Calvin wewe ndo uwe Alvin” walianza kubishana wale watoto wakigombania jina.. Nikatoa coin ya shilingi mia mbili kisha nikawaambia haya chagueni upande Samweli akachagua kichwa na Samsoni mwenge, nikawaambia nairusha juu upande utakaokuwa juu ndo ataitwa Calvin, nikairusha juu kisha ikadoka chini na upande wa kichwa ndo ilikua juu hivyo Samweli alishinda… “wewe utakua CALVIN na wewe utakua ALVIN sawa baba” “kwahiyo mimi C na wewe A” “Yap kweli kabisa C&A” AMINI USIAMINI, UKIMWI UPO NA UNAUA, ANGALIA MZUNGUKO HUU AMBAO UMEWAKUMBA HAWA AWTU, BABA MZEE AMBONILE,SOMOE,PRISCA NA ALVIN >>>>>>>>>MWISHOOOOOO
Posted on: Sat, 19 Oct 2013 08:02:19 +0000

Trending Topics



Recently Viewed Topics




© 2015