COCOJAMBO ASUBUHI HII: ALHAMISI, 28.11.2013: (HABARI). Kiajana - TopicsExpress



          

COCOJAMBO ASUBUHI HII: ALHAMISI, 28.11.2013: (HABARI). Kiajana mmoja aliyegundua umeme wa upepo zanzibar, aolalamikia wizara kwa ya sayansi na teknolojia kwa kumdharau na kumuibia wazo lake la kugundua umeme wa upepo...... Waziri wa Afya zanzibar JUMA DUNI ametoa maelekezo kwa idara husika katika wizara yake kwa kumsaidia kijana Haji Ally Haji aliyeanguka kwenye mkarafuu na kukosa huduma kwa zaidi ya miaka mitatu(3) hapa zanzibar.............. Viongozi wa vyama vya kisiasa nchini Ujerumani wamesaini makubaliano ya awali ya kuunda serikali ya mseto. Kansela Angela Merkel amesema serikali mpya ya nchi yake itasimamia Muungano wa utulivu....... Wizara ya ulinzi ya Mali imesema kuwa vikosi vya usalama vya nchi hiyo vimemkamata Jenerali Amadou Sanogo, aliyeongoza mapinduzi yaliyoitumbukiza Mali kwenye mzozo mwaka uliopita.... Mabingwa wa England, Manchester United, Usiku huu wametinga kwa kishindo kikubwa Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UCL baada ya kuitwanga Timu iliyo Nafasi ya Pili kwenye Bundesliga, Bayer Leverkusen, Bao 5-0 wakiwa Nyumbani kwao huko Germany...... MTANGAZAJI; JACKSON SEKIETE
Posted on: Thu, 28 Nov 2013 04:06:44 +0000

Trending Topics



px; min-height:30px;"> BISMILLAHI RAHMANIRAHIM Im not married but I know marriage how
Title, All Are One: A Lovecraftian inspired college story.

Recently Viewed Topics




© 2015