Hujambo Karibu tena kwa matangazo ya AMKA na BBC asubuhi ya leo nami Dinah Gahamanyi ambapo miongoni mwa yale tunayokuandalia ni pamoja na: Wakimbizi wa kisomali karibu nusu milioni wanaoishi Kenya kurejea makwao, serikali ya DRC na waasi wa M23 watatia saini mkataba wa usitishaji mapigano hii leo na Kenya yaunga mkono kauli ya rais wa Tanzania Jakaya kikwete kuhusu mustakabali wa Jumuiya ya Afrika mashariki na kuiomba Tanzania isaidie kuunga mkono pendekezo la kusogezwa mbele tarehe ya kesi dhidi ya rais wa Kenya Uhuru Kenyatta. Na usisahau tutakuwa na spoti . Tupe maoni yako kupitia ukurasa huu. Tuko pamoja
Posted on: Mon, 11 Nov 2013 02:25:02 +0000