Jamaa kapoteza mali zote na akawa maskini wa kutupwa kwa sababu ya ulevi. Siku moja asubuhi akawa anapita karibu na jalala akaona chupa tupu za bia. Akaishika ya kwanza akaipasua: kwa sababu yako nimeachana na mke wangu. Akaichukua ya pili akaipasua: kwa sababu yako nimeshindwa kusomesha wanangu. Akaichukua ya tatu akaipasua kwa hasira: kwa sababu yako nimefukuzwa kazi. Akaishika ya nne nayo akaipasua: kwa sababu yako nimeuza mali zangu zote hadi nimefilisika. Akaichukua ya nne ila akakuta imejaa bia na bado haijafunguliwa akasema: we kaa pembeni kwanza, huu ugomvi hata haukuhusu, tutaongea baadaye ila ole wako na wewe unifanye kama walivyonifanyia wenzako.
Posted on: Wed, 17 Jul 2013 13:26:40 +0000
Trending Topics
Recently Viewed Topics
© 2015