KUNA NYAKATI MTAGOMBA NA KUNUNIANA, ILA HAIONDOI UKWELI KUWA - TopicsExpress



          

KUNA NYAKATI MTAGOMBA NA KUNUNIANA, ILA HAIONDOI UKWELI KUWA MNAPENDANA..... Siku zote katika maisha yako, pambana kupata furaha. Ikitokea wewe na mwenza wako picha haziendi kutokana na tofauti za hapa na pale, wajibu wako ni kuirekebisha hiyo hali kwa haraka na mapema iwezekanavyo.... Si vyema kulimbikiza mambo yanayokwaza moyo bila kuyatafutia ufumbuzi... Yapo mahusiano yaliyovunjika si kwa sababu wahusika walikuwa hawapendani, bali wenyewe waliamua kulea migogoro na chuki zisizo na maana. Je sio kweli kwamba "Inauma sana kuachana na mtu unayempenda?" Naamini ni kweli kwa wengi wenu.... Uhusiano wa kimapenzi unahusisha moyo hivyo ni vyema kila siku ongea nae yeye na sio mtu mwengine, kisha jadili nae na uulize maswali mengi kadiri unavyoweza ili akupe majibu sahihi ya maswali yako.... Hakikisha unaweka pembeni tamaa, ongea naye na akwambie hitaji lake halafu fanyia kazi.....!
Posted on: Wed, 28 Aug 2013 07:41:18 +0000

Trending Topics



Recently Viewed Topics




© 2015