Kwa nini baadhi ya wanaopinga kuwepo kwa serikali tatu ndani ya muungano lazima waseme kuwa itawapa mzigo wa gharama wananchi? Hii ni kujaribu ku-win support yetu au vipi? Hawa hawajui kwamba sisi wananchi ndiyo tuliopendekeza hivyo kwa kuona kuwa wizara za sasa zisizo za muungano zitabaki kama zilivyo na kila kitu, majengo, magari, mfumo wa uongozi nk kwa gharama hizi hizi za sasa huku zile zitakazokuwa za muungano zitahudumiwa kama zinavyohudumiwa sasa? Rais wa Tanganyika awe kwenye ofisi ya sasa ya Dr. Ghalib Bilal,kwisha. Gharama za ziada,kama zitakuwepo, zitakuwa ndogo mno ikizingatiwa kuwa makamu wa rais wa shirikisho hatakuwepo. Wanaopinga serikali tatu wamuone Professor Issa Gulamhussein Shivji awape nondo zilizoshibishwa kitaalam kupinga idadi hiyo ya serikali na waache kupotosha gharama za ziada na kutishiana kwamba muungano utavunjika. Hoja hizi hazina mashiko kabisa. Za Professor Shivji za kimgongano wa utendaji wa vyombo vya serikali hizo ndizo za kujadilika.
Posted on: Mon, 24 Jun 2013 05:23:05 +0000