Mshambuliaji wa Yanga na timu ya Taifa (Taifa Stars), Mrisho - TopicsExpress



          

Mshambuliaji wa Yanga na timu ya Taifa (Taifa Stars), Mrisho Ngassa ameamua kulipa mwenyewe deni lake la Sh45 milioni anazotakiwa kuilipa klabu ya Simba baada ya kuhukumiwa na Shirikisho la Soka nchini (TFF). Awali Ngassa alikuwa ameweka ‘ngumu’ kulipa fedha hizo na kuzua tafrani kwa mashabiki na wanachama wa Yanga kuhusiana na adhabu yake ya kulipa fidia iliyotolewa na Kamati ya Sheria, Maadili na Hadhi ya Wachezaji ya TFF. Kamati hiyo ilimfungia Ngassa kucheza mechi sita, adhabu ambayo amekwisha itumikia na kilichobakia sasa ni #kulipa_fedha_hizo_ili_aweze_kucheza_mechi_za_Ligi_Kuu_ya_Tanzania Bara.
Posted on: Fri, 27 Sep 2013 11:20:25 +0000

Trending Topics



Recently Viewed Topics




© 2015