Mume wangu amenichanganya sana, siwezi hata kuwaza mambo mengine ya msingi, namuwaza yeye tu, nawaza nafika mwisho bila kupata suluhu, ndio maana ninaomba ushauri wenu Hivi karibuni tukiwa njiani kwenda kazini, akaniambia kuwa ameota anafanya mapenzi na mwanamke mwingine, (alinitajia jina la huyo mwanamke, ni mtu ninaemfahamu vizuri sana, tena mimi na huyo mwanamke wala hatuivi, kutokana na kuwa na mdomo mchafu sana, Sasa nashangaa na kujiuliza 1. Kwanini amuote yeye na asiniote mimi??? 2. Kwanini aniambie ndoto ya kipuuzi kama hii? 3. Aliniambia ili iweje 4. Ingekuwa mimi ndio nimwambie yey enimeota nafanya mapenzi na mtu anemfahamu ingekuwaje? Wadau naombeni ushauri wenu, ni jambo dogo bila kutafakari, ila ukilitafakari … inauma sana, ushauri please!!!! SHARE NA WASHKAJ WAJANJA #SNWW
Posted on: Sat, 28 Sep 2013 10:14:52 +0000