STORY....kasheshe la mama mwenye nyumba MTUNZI.....Cox dawa - TopicsExpress



          

STORY....kasheshe la mama mwenye nyumba MTUNZI.....Cox dawa yao Ilipoishia Tulifika salama na yule binti arusha tukaenda hotel kupumzika nikampigia simu rafiki yangu ili kumjulisha kuwa nimefika salama akaniambia afadhali nimepiga alikuwa ananitafuta mda mrefu nimemuachia majanga Endelea SEHEMU YA 66 Nilistuka sana kusikia msela wang ananiambia nimeacha majanga nikamuuliza "majanga gani tena rafiki yangu? Akaniambia"nilifika gheto mama nyumba akakuulizia nikamuambia umesafiri kidogo akalalamika sana kwann hujamuaga nikamuambia umepata safari ya dharura umeondoka ghafla akauliza mbna simu yako haipatikani nikamuambia upo sehemu mbaya"" nilimsikiliza sana kwa makini msela wangu huku nikiwa na hamu ya kujua hayo majanga aliyoniambia nimemuachia akaniambia" mama mwenye nyumba akasema kuna watu wamekuja kukuulizia kma mara tatu nikamuuliza wakoje akaniambia ni wakaka hivi walikuja na gari kwa haraka haraka nikajua tu lazima watakuwa watu wake jimama wako mm nikajifanya kma sijui lolote nikapotezea zile stori" daah nikajisemea afadhali nimewahi kuondoka wale watu wangenitia mikononi mwao basi nikamuambia msela wangu kesho yake nitamtafuta aniambie kinachoendelea huko mjini mda huo wote naongea nilitoka nje ya hotel ili yule binti asisikie maongezi yangu na msela wangu niliingia ndani kma kawaida yake yule binti alikuwa na wivu sana akaniuliza nilikuwa naongea na nani mda wote ule nikamdanganya pale nikampanga hadi akanielewa kwa kweli ile hotel tuliyofikia ilikuwa nzuri sana ilikuwa na kila kitu tuliinjoi sana yule binti akaniambia nijiandae siku hiyo tutoke tutembee tembee maeneo mengine mazuri nikayaone yani nilikula sana bata na yule binti lkn mda wote nilikuwa nawaza sana binti mdogo kma yule alizitoa wapi zile pesa sababu matumizi yetu yalikuwa makubwa sana tulikula sana bata tulitembea sehemu nyingi sana na nzuri za kifahari ambazo ktk maisha yangu sikudhania hata kma nitakuja kwenda sehemu kma zile nilikuwa nakunywa pombe kwa fujo sana ili mradi tu nipungize mawazo ya majanga yangu yote niliyoyaacha dar nilitamani hata yule binti aniambie tuishi pale hotel hata mwaka mzima nisirudi kabisa dar na swala la kurudi kijijini kidogo lilikuwa gumu sababu maisha ya kule yalikuwa ya hatari na tayari nilikuwa nimeshazizoea raha za mjini nikahisi nikirudi kijijini nitakonda sana Ilikuwa ni mida ya jioni nipo zangu na yule binti chumbani msela wangu akanipigia simu tukasalimiana akaniambia"yan msela wangu fanya tu haraka utume pesa nihame hapa gheto huyu mama jana kanifanyia mambo ya ajabu sana kma aliyokuwa anakufanyia wewe" nikastuka kidogo nikaguna nikamuuliza"majanga gani tena rafiki yangu? Akaniambia"jana nimetoka kazini mida ya jioni nimekaa zangu sebuleni naangalia movie akaja mama mwenye nyumba nikamsalimia nikajua labda ana shida akaniambia amekuja kuangalia muvi na mm lkn nikashangaa kaanza kuniambia habari ambazo hata sikumueleewa akaanza kunisifia huku anakukandia sana ww sababu ulishaniambiaga tabia yake nikawa nishamsoma mm nikawa napmpotezea akaondoka akaniambia atarudi mda si mrefu kweli mda si mrefu akarudi akiwa ndani ya khanga moja akaanza kuniambia anataka nifanye naye mapenzi mm nikawa nakataa lkn akawa ananilazimisha huku ananiahidi vitu kibao" nilimsikiliza huku nasikitika sana kwa kitendo anachofanya yule mama mwenye nyumba yani alinilazimisha mm nifanye naye mapenzi nikamkubalia mimi nimeondoka kaanza tena kumtaka rafiki yangu ninayeishi naye kwa kweli roho iliniuma sana Lkn bahati mbaya wakati rafiki yangu bado hajanimalizia stori yule binti akatokea nikakata simu haraka haraka akaniuliza"vipi bby mbna sikuelewi ulikuwa unaongea na nani mbna umeniona mm umekata? Nikamwambia"nilikuwa naongea na rafiki yangu bby namuuliza habari za dar? hakuniamini kabisa alionyesha kuwa na wasiwasi na mm akaniambia"bby unanidanganya kma rafiki yako kweli mbna umeniona mm umekata simu haraka hebu nipe simu yako nihakikishe" yani simu yangu ilikuwa na message za ajabu nikajua nikimpatia itakuwa balaa kulikuwa na message za yule demu wangu wa saluni kibao tunaongelea ile mimba yake nikaona sasa akizisoma nitaharibu kila kitu Itaendelea Kesho saa 1 jioni GONGA LIKE KAMA UMEIPENDA HII STORY
Posted on: Wed, 17 Jul 2013 18:05:45 +0000

Trending Topics



Recently Viewed Topics




© 2015