Sisi hata ile posho ya sh.moja kwa siku hatuna. Nimetoka benki za NBC & CRDB Kuomba mkopo wa biashara sh.30,000,000 kuendeleza Pro Audio Light Tanzania nimenyimwa inasikitisha sana. Je benki za serikali zinakopesha kina nani au ndiyo undugu naizesheni na kutowathamini watu wa kipato cha chini na hasa kutoendeleza vipaji vyao? Serikali ikiendelea kufanya hivyo inatunyanyasa sisi wananchi wa chini iweje viongozi hasa wabunge wapewe pesa kama hizo wakati mwnanchi wa kipato cha chini hana kitu ni ugandamizaji usio na usawa. Tumekuwa tukishuhudia mijadala ya ungomvi katika mikutano Bungeni na si mijadala ya kuendeleza wananchi wanaowakilishwa kwa maendeleo yao na Nchi huo ni wizi mnatuibia na hii haikubaliki hata kidogo.
Posted on: Thu, 24 Oct 2013 12:00:11 +0000