Uliaaplai kazi mwaka juzi, jiii, ukasubiria mwaka jana, jiii, mwaka huu jiii, dakika za mwisho za mwaka uishe, ushajisongea zako mbele kwa mbele eti jana ndo wanakuita, afu simu wanakupigia jioni wanakwambia uende leo asbuhi. Wao imewachukua miaka mi3 kukuita, ila wanataka wakupate ndani ya masaa machache bila kujali upo Dar ama Mkoa, unaumwa, umefiwa ama la! Wenye vyeo maofisini wekeni utu mbele, sio kwa vile nyie mshapata kazi basi mnaburuza watafutaji ajira. Afu kwanza hiyo kazi gani ya haraka hivyo au kuna bomba limepasuka ofisini mnatafuta fundi?
Posted on: Tue, 12 Nov 2013 11:03:53 +0000